COACH SAID KWIMBI OF JANG'OMBE BOYS FC AWAKENING HIS PLAYERS

Jang'ombe Boys FC players who are coaching by their new coach Said Kwimbi have been given a awakening of the whole issue of football game discipline.

Speaking during the training of the team today in training ground, Kwimbi has told the players that in order to become successful in anything; they have to choose discipline as a compass and direction toward that matter.






"My dear brothers, my children and my friends, if you really have choosen football intentionally as a part of your life, then make sure you switch on your discipline to the peoples, either  a young or an old, whether in the field during the exercise, during the match and even you walking on the streets, because discipline is everything in the human life, so even in the football game, you have to reserve it’s right in the  disciplinary matters, if you’ll do so then the football also shall reserve your rights, and vice versa is true ".

"What I can say,  this team has been well decorated with great players, but I can assure you, in the football even if  you are a star, you can show how to kick the ball  by using your teeth, but if you are lacking in discipline you are nothing, the football family recognizes the disciplinary player as their best player at all time, when I’m talking about discipline doesn’t mean that you have to helps people carrying their loads on the streets only, no, but you have to follow Dos and Don’ts of Football"said Kwimbi.

Jang'ombe Boys FC will play its second friend match since closing the Zanzibar transfer window, but for Coach Kwimbi this is his first game since he took place as a coach of the club.

Jang'ombe Boys FC took this chance to invites you all to this match to eyes witness yourelves our new  talent squard this season, the entrence fees is sh.1,000 / - and sh.2,000 / - only, you are warmly welcome



KOCHA KWIMBI AAWAPA NASAHA WACHEZAJI WA JANG'OMBE BOYS FC.

Wachezaji wa timu ya Jang'ombe Boys FC ambao kwa sasa inafundishwa na kocha wao mpya Said Kwimbi wamepewa nasaha juu ya suala zima la nidhamu ya mchezo wa mpira wa miguu.

Akizungumza wakati wa kufunga mazoezi ya timu hio leo katika uwanja wa mazoezi wa timu hio, Kocha Kwimbi amewaeleza wachezaji hao kwamba ili ufanikiwe katika kitu chochote basi ni lazima nidhamu iwe ndio dira na kitu cha mbele katika kitu hicho.

"Ndugu zangu, watoto wangu na marafiki zangu wachezaji, kama kweli nyinyi mmechaguwa mpira kuwa ni sehemu ya maisha yenu, basi muhakikishe mnatunza nidhamu kwa wakubwa na wadogo, iwe uwanjani wakati wa mazoezi, wakati wa mechi na hata mtaani, kwa sababu nidhamu ndio kila kitu katika maisha ya mwanadamu, hivyo hata katika huu mpira wa miguu basi unatakiwa kuutendea haki katika suala zima la kinidhamu, ukifanya hivyo basi na wewe mpira utakutendea haki tu".

"Niseme timu hii imebahatika kuwa na wachezaji wazuri sana, lakini nataka niseme hata uwe "Star" unapiga mpira mpaka kwa meno lakini kama huna nidhamu basi mchezaji wa maana, familia ya soka inamtambua yule mwenye nidhamu kuwa ndio mchezaji bora, na ninapozungumzia nidhamu simaanishi kwamba ukiona mtu ukapokee au umuamkie shikamoo au chei chei, laa hasha! nidhamu ya mpira ni kuhakikisha kwanza unafanya yale walimu na timu inayataka na unayaacha yale ambayo walimu na timu haiyataki" alisema Kwimbi.



Wachezaji, viongozi na wadau wakisikiza
nasaha za Mwalimu baada ya mazoezi.


Kuelekea mchezo wa kirafiki kati ya Jangombe Boys FC na Villa United FC (Mpira Pesa) hapo kesho tarehe 21 Septembe 2017 saa moja za usiku katika Uwanja wa Amani, Kocha Kwimbi aliwataka wachazaji wote 30 ambao wamesajiliwa na timu msimu huu kufika kwa wakati klabuni ili timu nzima ifike pamoja kiwanjani kwa jaili ya mchezo huo wa kirafiki.

"Nidhamu ni uwanja mpana sana, hivyo nikizungumzia nidhamu basi ni pamoja na wachezaji wote thelathini waliosajiliwa na timu na wanaohudhuria mazoezi, basi wote wafike mapema eneo husika ili sote tuwepo pamoja kucheza mchezo huo, kwa sababu siku ya kesho tunahitaji kuwatumia wachezaji wote, ili tuweze kurekebishana makosa na hatimae tufanye vizuri katika ligi" alimalizia Kocha Kwimbi.

Jangaombe Boys FC itacheza mchezo wake huo ukiwa ni wa pili tangu dirisha la usajili kufungwa, lakini utakuwa ni mchezo wa mwanzo kwa Kocha Said Kwimbi tangu achukuwe mikoba ya kuinoa timu hio.


Jang'ombe Boys inawakaribisha nyote kuja kuona kikosi chetu kipya kilichosheheni kila aina ya vipaji msimu huu, kiingilio ni sh.1,000/- na sh.2,000/-.

Maoni