Timu ya Jang’ombe Boys FC inayoshiriki liki kuu kanda ya
Unguja usiku wa leo wameiyayusha timu ya Shaba FC inayoshiriki ligi kuu kanda ya
Pemba kwa kuifunga magoli manne bila ya majibu, ni Jangombe Boys walioonekana kuumiliki mpira na kucheza kwa kasi kubwa sana, kujiamini
na maelewano sambamba na kupeana pasi za uhakika tangu dakika ya mwanzo wa mchezo, kitendo ambacho kiliwafanya vijana hao wa Kojani Pemba kupoteana, ambapo
Jang'ombe Boys iliwachukuwa dakika 19 tu wakaandika goli la kwanza lililofungwa
kwa njia ya penalti na mchezaji Suleiman Ali Suleiman (Pichori) aliyetua klabuni
hapo akitokea klabu ya Kilimani City yenye makao yake katika Magorofa ya
Kilimani Zanzibar.
Katibu Friends of J.Boys, akikabidhi
Cheti cha mchezaji bora wa mechi
kwa mchezaji Hassan Choum.
Jang’ombe Boys hawakuridhika na goli hilo walionekana
kuzidisha kasi Zaidi na dakika tatu baadae mnamo dakika ya 21 Helfini Salum
(Fini) aliyesajiliwa kutoka Kilimani City akaiengezea timu yake goli la pili
kuunganisha krosi kali ilichongwa na Hassan Chumu (Mbungi).
Shaba walizidi kuelemewa na vijana hawa wa Jang'ombe Boys na
dakika ya 33 Mustafa Vuai Hassan (Tafa-Neimar) akaingezea goli Jangombe Boys
goli la tatu la kuongoza, goli ambalo lilidumu hadi dakika ya 56 Tafa akawanyanyua
tena washabiki wa Jang’ombe Boys kushangiria goli la nne.
Wachezaji wa Jang'ombe Boys wakinyosha
viungo kabla mchezo wao na Shaba.
Dakika 59 Shaba walionekana wangepata goli baada ya beki
kisiki wa Jang’ombe Boys Ali Humudi Bardu (OCD) kuteleza na kuanguka wakati
akiburura mpira na mpira ukaingia miguuni mwa mshambuliaji Wa Shaba, mshambuliaji huyo alipiga shuti kali ya
chini, ambapo ni dhahiri kama si umahiri na uhodari wa golikipa nambari moja wa
Jang’ombe Boys Hasham Haroun Ruga kuonyesha umahiri wake na kuufuata mpira huo
na kuudaka, basi ilikuwa ndio nafasi pekee ya wazi kwa timu ya Shaba kuandika
goli la kufutia machozi.
Dakika 72 baadae golikipa wa timu ya Shaba aliyeingia
Kipindi cha pili alifuta goli la wazi kwa kuokoa mpira wa kichwa uliopigwa na
Hassan Seif Banda aliyesajiliwa kutokea Taifa ya Jang’ombe ambaye aliingia
kipindi cha pili kuchukuwa nafasi ya mshambuliaji mwenzake Abrahman Othman
(Chinga) aliyesajiliwa kutokea klabu ya Singida United ya Mkoani Singida, hadi mwisho Jang’ombe Boys FC 4-0 Shaba.
Katika upande mwengine jopo la makocha waliokuwa wakifuatilia mchezo huo wamemchagua Hassan Choum Abdallah kuwa ndiye mchezaji bora wa mechi hio yaani "Man of the Match", ikumbukwe kwamba Hassan Choum alishawahi kutangazwa mchezaji bora na 'FRIENDS OF J. BOYS' na akakabidhiwa cheti maalum pamoja na fedha.
Katika upande mwengine jopo la makocha waliokuwa wakifuatilia mchezo huo wamemchagua Hassan Choum Abdallah kuwa ndiye mchezaji bora wa mechi hio yaani "Man of the Match", ikumbukwe kwamba Hassan Choum alishawahi kutangazwa mchezaji bora na 'FRIENDS OF J. BOYS' na akakabidhiwa cheti maalum pamoja na fedha.
Maoni
Chapisha Maoni