MAKOCHA JANG’OMBE BOYS: Hakuna kurudi nyuma.


Kufutia kufungwa katika mchezo wa leo Makocha Jang'ombe Boys wamewataka wachezaji wao kutorudi nyuma.

Kocha mkuu wa Jang’ombe Boys Said Kimbi amewataka wachezaji wake kuyakubali matokeo ya mchezo uliomalizika kati ya timu yake dhidi ya timu ya Black Sailor, ambapo katika mchezo huo Black Sailor wameweza kuifuga Jang’ombe Boys kwa goli moja lililofungwa dakika ya 75.
Akizungumza na mtandao huu baada ya kumalizika kwa dakika 90 za mchezo huo, kocha Kwimbi amesema hakuna mabadiliko yatakayobadilika katika mchezo wa mpira wa miguu Zaidi ya kushinda, kutoa sare na kushindwaa.
Kikosi cha Jang'ombe Boys 

“Binafsi matokeo nimeyakubali ingawa yanaumiza, hivyo nawasihi wachezaji wangu pia wayakubali matokeo na wayapokee matokeo haya, kwani katika mpira a miguu zitakazobadilika ni sharia tu, lakini matokeo ni haya haya, kushinda, kutoa sare na kufungwa, umuhimu wa kuyakubali matokeo kama haya yatatusaidia kujipanga upya, kufanya ‘touch up’ (masahihisho) na hatimae kufanya vyema katika michezo ijayo, ukizingatia ligi bado ina safari ndefu.

“Hakuna jinsi ya kuyageuza matokeo baada ya dakika 90 za mchezo, njia pekee ya kuyageuza matokeo ni kushinda michezo ijayo, hakuna wa kumlaumu kwa sababu sote tulijitayarisha ili tushinde lakini mpira ndio hivyo niseme ni mchezo wa ajabu ka sababu pale unapotegemea matokeo fulani ndipo unapata yale matokeo usiyoyataraji” alimalizia Kocha Kwimbi.

Kwa upande wa Kocha msaidizi wa timu hiyo kocha Issa Othman (Amasha) amesema licha y kupoteza mchezo wa leo bado anaamini kwamba bado timu yake ina kikosi bor Zaidikatika msimu huu, hivyo hakuna cha kukatisha tamaa na kuitoa timu yake katika malengo yake.
Akizungumz na mtandao huu, kocha Amasha amewataka wachezaji wake kuyapokea matokeo haya ili iwe ndi chachu y kufanya vyema mchezo unaofuata.

“Niseme kwamba hakuna timu isiyofungwa, kila timu lazima ipitie matokeo kama haya, iwe mwanzoni au mwishoni, hivyo anaelia mwanzo atacheka mwisho na anaecheka mwanzo atalia mwisho, niwambie wachezaji kwamba ‘Hakuna kurudi nyuma’, matokeo kama haya si mageni kwetu ikumbukwe hata ligi iliyomalizika tuliharibu michezo mitano mfululizo lakini angalieni tulipojiuliza na tukarekebish na tukatengeza ari zetu, nyinyi wenyewe mliona kilichotokea, naamini tukifanya kazi kwa pamoja tutacheza nane bora na hatimae kupata ubingwa” alisema Amasha.


Mchezo unaofuata unategemewa kuchezwa tarehe 24/10/2017 dhidi ya Chuoni FC, mchezo amabo utasukumwa katika dimba la uwanja wa Amani saa 10.00 alasiri.

Maoni