Viongozi, wachezaji
na wadau wote wa Jang’ombe Boys FC inayonolewa na Kocha Saidi Kwimbi, wamesema
mchezo wa kesho “Ama faimaa” lazima timu yao ishinde mchezo huo ili kuiweka
timu katika mazingira ya matumaini na kurejesha matumaini kwa washabiki wake.
Na: Ali Mohammed.
VIONGOZI WATOA NENO ZITO:
Katibu wa Jang’ombe Boys Abdalla Mahfodh amesema kwamba kawaida ya timu hii huanza kwa kuharibu katika misimu yote ya ligi kunzia tangu madaraja ya chini, lakini utamaduni huu umeanza kuomekana kuwa haukubaliki tena katika timu hii, kwani ligi ya mara hii inaonekana haitatoa nafasi ya timu zilizoharibu mwanzoni kujirekebisha mwishoni.
Katibu wa Jang’ombe Boys Abdalla Mahfodh amesema kwamba kawaida ya timu hii huanza kwa kuharibu katika misimu yote ya ligi kunzia tangu madaraja ya chini, lakini utamaduni huu umeanza kuomekana kuwa haukubaliki tena katika timu hii, kwani ligi ya mara hii inaonekana haitatoa nafasi ya timu zilizoharibu mwanzoni kujirekebisha mwishoni.
“Imekuwa kama ndio
utamaduni wetu kuharibu mechi kama tano hadi sita hivi halafu tena baada ya
masahihisho ya makosa yetu huwa tunakaa sawa na kuanza kukusanya matokeo
mazuri, lakini utamaduni huu haupendezi na wala hautoi dhamana katika ligi ya mwaka huu sioni kama kutakuwa na nafasi ya timu zilizoharibu mwanzoni kujisahihisha katikati au
mwishoni, hivyo michezo mitatu inatosha sana na sasa hatutaki tena kuendelea na
utamaduni huu na kesho Insha Allah ndio mwisho.
“Nasema hivi kwa
sababu mwaka huu timu zinazoshiriki ligi ni timu 14 Pemba na 14 Unguja timu
zinazoshuka Unguja ni 6 na Pemba ni sita, kwa hio kil timu imejipanga kuchukuwa
alama mwanzoni, hivyo kama wewe umekosa mwanzo na mwenzako aliyekosa mwanzo
haitakuwa rahisi kupata mwisho kwa menzio aliyekosa mwanzo kama wewe. Alisema
Katibu Mahfoudh.
Kwa upande wa Rais wa
timu Ali Othman Kibichwa, amesema kama ilivyolazima kufa kwa binadamu, basi
ikiwa timu tunataka ikae katika mazingira ya kuonyesha kwamba tunatafuta
nafasi, basi lazima timu itoke na alama zote tatu na si vyenginevyo.
“Kesho kama tunataka
kuiweka timu yetu katika mazingira ya kutafuta nafasi katika ligi, basi ushindi
ni muhimu na lazima 'kama ilivyokufa na binadamu', matokeo yeyote kinyume na ushindi ni
kusema tunaendelea kupoteza nafasi au tunajiweka katika mazingira magumu katika
kutafuta nafasi.
“Maandalizi ya mchezo
yamekamilika vizuri, tayari timu imeingia kambini ikiwa na wachezaji 29 na
wachezaji wana ari na mchezo na wametuahidi ushindi sisi viongozi na washabiki na
wewe ndugu mwandishi ukiwa shahidi. Alisema Ali Othman.
MAKOCHA WANG’AKA:
Kama tujuavyo Jang’ombe
Boys FC mwaka huu imesajili kocha Said Kwimbi ambaye kabla aliwahi kufundisha
timu ya Kilimani City, hivyo kuna mengi yanzugumza na Kilimani City, kuna
shutuma za kwamba eti hata wachezaji waliosainiwa na Jang’ombe Boys wamejiunga
hapa kwa ushawishi wa Kwimbi, jambo ambalo kwimbi mwenyewe amelipinga vikali
sana.
“Kesho tunacheza
mchezo wetu wan ne ambao ni rahisi lakini ni mgumu na nitawaeleza kwa nini ni
mgumu, kuna shutma dhidi yangu kwamba eti hawa mabwana, Pichori na Fini kwamba
nimewaleta mimi katika timu, kitendo ambacho mimi sikikubali, kwa sababu Issa
anajuwa kwamba mimi nilishasema kwamba kwa kipindi hichi sitaki kujihusisha na
ukufunzi wa mpira, lakini Issa ndio akaniomba nije tusaidiane baada ya yeye
kupata fununu za kocha Maha kujiunga na Miembeni City, lakini kauli yangu hii
haikubaliki ndani ya Kilimani City.
“Hizi timu zina
visasi vyao tangu huko chini, hivyo visasi hivi vitaendelea na kesho ndio siku
yenyewe ya visasi kuendelea, ila mpia dakika 90 lakini timu yangu naiamini na
natosheka kuamini kwamba kesho ndio ligi kiupande wetu Insha Allah tutaianza
kwa matokeo yatakayotuonda hapa tulipo na kutusogeza kuelekea kule tunakokutaka
ambako ndiko mahali timu hii inastahiki kuweka maskani kimsimamo. Alisema
Kwimbi.
Nae Kocha Msaidizi
Issa Othman (Amasha) amesema, anajuwa uhasama uliopo baina ya timu hizi,
anajuwa hasira walizo nazo kilimani City baada ya kuwachukuwa wachezaji wake
wawili katika usiku wa mwisho a dirisha la usajili.
“Najuwa uhasama wa
kimchezo baina yetu na Kilimani City, najuwa jinsi gani tulivyowavuruga
tulipowasajili Helfeni na Suleiman (Pichori), hasa kitendo cha usiku wa mwisho
wa kufungwa kwa dirisha la usajili, ile ilikuw bakora kubwa na mbaya sana,
hivyo mchezo ni mgumu lakini ushindi mechi hii ni lazima” Alisema Amasha.
KAPTENI NAE AKAZIA:
Mbali ya viongozi hao
waliotangulia kuwahakikishia wadau wa Jang’ombe Boys kwamba timu itafurahisha
katika mchezo wa kesho, nae Kepteni wa timu Ibrahim Mohammed (Sangula) hakuwa
mbali na mwandishi wa mtandao huu aliyekuepo uwanja wa mazoezi wa timu hiyo ili
kuzungumzia mchezo huu nae alieleza haya:
“Baada ya kupokea
ahadi nyingi kutoka kwa wadau wetu, na mimi nashawishika na kulazimika kusema
kwamba, wachezaji wenzangu wote tumeshainingia katika mchezo huu na iliyobakia
baada ya wiki kadhaa za kusuwa suwa.
“Nadhani pale pembeni
unaona shehena ya mapegi, yale ni mabegi ya wachezaji sote 29 tuliosajiliwa na
timu hii kwa msimu huu, hivyo kuna tafauti kubwa sana ukilinganisha na michezo
mitatu iliyopita, michezo iliyopita hatukuwa tukiingia kambini sote lakini
kuanzia sasa tumeshikamana kwa pamoja ili kuleta ushindi katika kila mechi
kuanzia hii ya kesho.
“Hivyo nawambia City
majirani, ndugu zetu wajitayarishe na mateso ya kesho panapo majaaliwa,
tunajuwa tumejiandaa lakini mtiti huu kesho hakuna kuni ya nyongeza, tunapanga
magogo ya uhakika hata “Bulldozer” hlitaweza kuondoa magogo hayo, na jambo zuri
hata makocha wetu kwa mchezo huu leo tunondoka nao kuingia kambi, hii itasaidia
kumaliza mchezo mapema sana Insha Allah. Alimaliza Sangula.
KUMBUKUMBU ZA MICHEZO
ILIYOPITA:
Timu hizi kwa
kumbukumbu za michezo minne ya karibuni yanaibeba Jang’ombe Boys FC, ambapo mchezo
wa kwanza katika mine hiyo Jang’ombe Boys walishinda 2-1 ka magoli ya Edo na
Rais, mchezo wa pili tukatoka sare ya goli 3-3 magoli ya Jang’ombe Boys
yalifungwa na Chinga, Beka Raul na Eddo, mchezo wa tatu tukwafunga kilimani
City 1-0 kwa goli la Kilahe na mchezo wa mwisho katika uwanja wa fuoni
tukitumia kikosi ‘B’ City walishinda 2-1.
Kwa niaba ya
wafanyakazi wa mtandao huu, tunaiombea timu yetu Jang’ombe Boys FC ushindi wa
kishindo katika mchezo huo mkali na wa kusisimua dhidi ya Kilimani City.
AMIN
Maoni
Chapisha Maoni