Wakati Kapteni wa
timu yetu Ibrahim Mohammed ‘Sangula’ akiwa katika shukrani za kumshukuru Mwenyezi
Mungu kwa kumjaalia kutimiza umri alionao kwa salama na uzima wa afya, mtandao huu
umegunduwa kwamba siku ya leo Ibrahim hayuko peke yake katika kusherehekea siku
hiyo bali kuna watu kadhaa ambao muda huu na wao wamo katika sherehe, dua na
maandilizi mengineyo ya kuadhimisha siku hio.
Mtndao huu umebaini
kwamba leo ndio siku ambayo mama mzaa chema wa nyota huyu alipomleta duniani
baada ya kupitia ukuta wake wa ‘facebook’ na kuona maandishi ynayoashiria uwepo
wa siku hii, katika ukuta wake huo ameandika hivi:
"Nashukuru mungu kwa kunijalia kunifikisha tena siku yangu ya
leo ya kuzaliwa me hakuna. mwenye uwezo huo isipokuwa ni yeye pekee pia na
nawshukuru wazazi wangu kwa kulea vizuri na kunitunza pia naishukuru familia
yangu kwa kuishi pamoja kwa mapenzi pia nawashukuru marafiki zangu wote na
maadui zangu kwa siku ya leo kuzaliwa kwangu nawapenda sana happy birthday to
me" aliandika Sangula.
Ndipo mtandao huu ukagunduwa kwamba, siku ya leo pia ni siku ambayo wamezaliwa watu wengi mashuhuri na maarufu akiwemo muimbaji SHAGGY kutoka JAMAICA pia wamo wanasiasa, wachezaji mpira, waimbaji, wanaharakati na wengine mbalimbali.
Wanasiasa:
John Shadegg, Gavana wa zamani wa jimbo la Arizona - Marekani
Bill Owen, Gavana wa Colorado - Marekani
Seif Sharrif Hamad, Katibu Mkuu a CUF - Tanzania.
Patrick Mc hendry, Congress Califonia.
Harry Moniba, Makamo wa Rais wa Zamani wa Liberia.
Joaquim Cissano, Rais mstaafu wa Zambia
Makocha:
Arsene Wenger, Arsenal FC
Brad Stevens, Reading, Sligo Rovers, Nothern Ireland, Fulham, Wycombe Wanderers nk
Wachezaji Mpira:
Michael Salgado, Mchezaji wa zamani wa hispania
Otis Smith, Mchezaji a zamani wa marekni
Andre palop mchezaji wa zamani wa hispania.
Ichiro Suzuki, mchezaji wa zamani wa Japan.
Chaswe Nsofwa, mchezaji wa zamani wa Zambia
Doni, Mchezaji wa zamani wa Brazil.
Orodha hio fupi ni miongoni mwa watu mashuhuri, lakini orodha hio si ukamilifu wa watu mashuhuri waliozaliwa siku ya leo sambamba na nyota wetu Ibrahim Mohammed (Sangula), bali hao ni wachache sana, miongoni mwao wameshatangulia mbele ya haki.
Kwa niaba ya timu nzima na wadau wote wa mtandao huu tunaungana na wote waliomtakia siku njema ya kuzaliwa.
"Happy Birthday to you"
Kwa niaba ya timu nzima na wadau wote wa mtandao huu tunaungana na wote waliomtakia siku njema ya kuzaliwa.
"Happy Birthday to you"
Maoni
Chapisha Maoni